DAR-Wananchi mbalimbali wameendelea kutembelea katika banda la Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na tsasisi zake ili kupata elimu kuhusu utekelezaji wa majukumu ya ofisi hiyo katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa maarufu kama SABASABA yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
Aidha, wameonesha kuridhishwa na huduma zinazitolewa na ofisi hiyo pamoja na mambo mengine wamepata elimu kuhusu masuala ya vijana, ajira ulemavu na Uratibu wa Shughuli za Serikali.Maonesho hayo kwa mwaka huu yana Kauli Mbiu inayosema “Maonesho ya Biashara ya Kimataifa sabasaba, Fahari ya Tanzania” tarehe 03 Julai, 2025.












