Waziri Dkt.Nchemba afanya mazungumzo na Ujumbe kutoka Kampuni ya Minara Tanzania

WAZIRI wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba amekutana na kufanya mazungumzo na Ujumbe kutoka Kampuni ya Minara Tanzania, ulioongozwa na Makamu wa Rais wa Kampuni hiyo, Bw. Richard Cane, ambapo pamoja na mambo mengine wamejadili namna ya kuendeleza ushirikiano katika kukuza Sekta ya Mawasiliano nchini.
Mkutano huo umehudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, Makamu wa Rais wa Kampuni ya Minara anayesimamia nchi za Afrika na Asia, Bw. Nicholous Vane, pamoja na wajumbe wengine kutoka Wizara ya Fedha na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na Kampuni ya Minara Tanzania.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news