CHAUMMA yazindua kampeni kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 29,2025

DAR-Leo Agosti 31,2025 jijini Dar es Salaam, Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) kimezindua rasmi kampeni kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais, wabunge na madiwani unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29,2025.
Katika uzinduzi huo, Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupita Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalim amesema,iwapo Watanzania watawapa ridhaa ya kuongoza nchi wanatarajia kutekeleza mambo mbalimbali ikiwemo maboresho ya tasnia ya habari nchini.
Vilevile katika eneo la utumishi wa umma amesema, atahakikisha nidhamu kwa kila mtumishi na kuwaboreshea maslahi yao kwa kuanza na msharaha wa kima cha chini shilingi 800,000 baada ya makato ya kodi.
Mbali na maboresho katika sekta nyingine ikiwemo ya afya na huduma za afya, pia amesema Serikali yake itahakikisha inaongeza nguvu kwenye sekta ya kilimo ili kuongeza uzalishaji wa chakula na kuwezesha kuwa na uhakika wa chakula na mazao ya biashara kote nchini.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news