Magazeti leo Agosti 2,2025

MBUNGE wa Viti Maalum anayemaliza muda wake na Msanii, Khadija Taya (Keisha) ameshindwa kufurukuta katika kura za maoni kupitia Jumuiya ya wazazi Tanzania Bara yenye nafasi moja baada ya kupata kura 94 kati ya kura halali 708.
Katika kundi hilo lililokuwa na wagombea 18, Catherine Joachim alipata kura 567 kati ya kura halali 708. Kwa upande wa Zanzibar, Mbunge wa viti maalum, Najma Murtaza Giga ameongoza kundi hilo baada ya kupata kura 591 na kuwaacha mbali wapinzani wake watano.

Katika kundi la wabunge wa viti maalum kwa wajumbe wa baraza la wawakilishi lenye nafasi mbili aliyeongoza ni Aza Januari Joseph aliyepata kura 350 kati ya kura halali 702 na Salama Abasi Juma aliyepata kura 330. Kundi hili lilikuwa na wagombea nane.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news