Magazeti leo Agosti 23,2025

WAZIRI wa Kilimo, Hussein Bashe meiagiza Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) kwenda kuwakamata na kuwafungulia mashitaka wauzaji wa pembejeo bandia ikiwemo mbegu za kilimo kwa mujibu wa sheria.
Bashe ameeleza hayo Agosti 22, 2025 mkoani Dodoma wakati akizindua Bodi ya Wakurugenzi ya TOSCI ambapo ameitaka kwenda kushirikiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) katika kupambana na tatizo hilo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Dk. Lilian Shechambo ametaja vipaumbele mbalimbali ambavyo bodi hiyo itakwenda kuvitekeleza ikiwemo kuendelea kuimarisha shughuli za usajili wa watoa huduma za mbegu (Seed Dealers) kwa kutoa mafunzo, ukaguzi na miongozo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news