Magazeti leo Agosti 27,2025

MKURUGENZI Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Crispin Chalamila amewataka wanasheria wa taasisi hiyo kuwadhibiti baadhi ya wagombea watakaobainika kutoa rushwa katika kipindi hichi cha uchaguzi kwa kufanya uchunguzi wa kina na wenye tija.
Chalamaila alitoa agizo hilo wakati akifungua mafunzo ya kuimarisha weledi wa taaluma ya sheria kwa wanasheria zaidi zaidi 300 wa taasisi hiyo kutoka mikoa yote nchini yaliofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere Mjini Kibaha mkoani Pwani.

Alisema, majukumu makuu ya taasisi hiyo ni kutoa elimu ya rushwa kwa umma, kuzuia rushwa na kufanya uchunguzi na kwamba katika kipindi hichi cha uchaguzi ni wanasheria hao wanajukumu kubwa la kuchunguza vitendo vya rushwa na kudhibiti hatua itakayosaidia upatikanaji wa viongozi bora.

"Sasa tunaelekea katika kipindi cha kampeni ambacho kitachukua miezi miwili, ni wakati wenu kufanyakazi ili kuchunguza vitendo vya rushwa ni dhahiri kwamba viongozi ambao wanaopatikana kwa njia ya rushwa ni ngumu kuwa viongozi bora hataweza kutusaidia kusimamia miradi,"alisema.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news