Magazeti leo Agosti 28,2025

BARAZA la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) limetoa mafunzo kwa Maafisa wa Uthibiti Ubora, Wakuu wa Vyuo na Wakuu wa Idara kutoka vyuo vya elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi katika Kanda ya Mashariki, kwa lengo la kuongeza ufanisi katika usimamizi wa vyuo hivyo na kuhakikisha ubora wa mafunzo unaboreshwa ili kuzalisha wahitimu wenye sifa zinazohitajika katika soko la ajira.
Akizungumza Agosti 27, 2025 jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Uthibiti Ubora kutoka NACTVET, Dkt. Jofrey Oleke, amesema kuwa mafunzo hayo yanalenga kuboresha ubora wa elimu inayotolewa katika vyuo vinavyosimamiwa na NACTVET, hususan katika maeneo ya utoaji wa elimu na uandaaji wa mitaala.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news