TAASISI ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) imejivunia kutimiza malengo matano ya msingi iliyojiwekea, likiwemo eneo la utafiti na ubunifu, pamoja na usimamizi madhubuti wa programu za uatamizi wa teknolojia.
Akizungumza Agosti 28, 2025 jijini Arusha wakati wa Mahafali ya 11 ya taasisi hiyo, Makamu Mkuu wa Taasisi, Prof. Maulilio Kipanyula, alisema taasisi hiyo imepanua wigo wake wa kitaaluma kwa kutoa Shahada ya Umahiri katika Ubunifu na Usimamizi wa Ujasiriamali kupitia Shule Kuu ya Mafunzo ya Biashara na Sayansi za Jamii (BuSH), ambapo wahitimu wa kwanza kutoka shule hiyo walitunukiwa shahada kwa mara ya kwanza.
Jumla ya wahitimu 111 walitunukiwa shahada katika mahafali hayo, ambapo 71 walitunukiwa Shahada ya Umahiri na 40 walitunukiwa Shahada ya Uzamivu.
Prof. Kipanyula alieleza kuwa dhana ya kubiasharisha bunifu na teknolojia inayoendelezwa na NM-AIST inalenga kusaidia Serikali katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, hususan katika kukuza viwanda na uchumi wa nchi kwa ujumla.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo































