Magazeti leo Agosti 31,2025

MKOA wa Geita unatarajia kupokea Mwenge wa Uhuru Jumatatu ya Septemba 01, 2025 katika kijiji cha Rwezera ukitokea Mwanza.
Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martine Shigella ametoa taarifa hiyo Agosti 30, 2025 wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea mapokezi ya Mwenge wa Uhuru.

Shigella amesema kwa mwaka 2025 Mwenge wa Uhuru ukiwa mkoani Geita unatarajia kupita na kukimbizwa katika jumla ya miradi 61 yenye thamani ya sh bilioni 164.4.

Amesema mwaka 2024 mwenge wa Uhuru ulikimbizwa ndani ya mkoa wa Geita na kuweza kufikia miradi 65 yenye jumla ya thamani ya Sh bilioni 32.2.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news