Magazeti leo Agosti 3,2025

MWONGOZO wa Kuanzisha na Kuendesha Shamba Darasa la Kilimo Biashara umezinduliwa rasmi Agosti 2, 2025 katika Kongamano la wadau wa kilimo lililofanyika sambamba na Maonesho ya Wakulima (Nanenane) katika Viwanja vya Nanenane, Nzuguni mkoani Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Gerald Mweli amesema mwongozo huo unaolenga kuwainua wakulima wa kawaida umezingatia vipengele mahususi ambavyo ni Uwezeshaji, Kilimo himilivu, Dhana ya biashara katika kilimo, Masuala ya usawa katika kilimo, kujikinga na magonjwa ya kuambukiza pamoja na uongezaji thamani katika mazao ya lishe,

Aidha, Katibu Mkuu huyo amewataka wadau wote wa sekta ya kilimo kuutekeleza mwongozo huo ili kuongeza thamani ya fedha katika sekta hiyo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news