Rais Dkt.Mwinyi awasili Dar

DAR-Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameondoka Zanzibar na kuwasili jijini Dar es Salaam tayari kushiriki Uzinduzi wa Harambee ya Kitaifa ya kuchangia Kampeni za Chama Cha Mapinduzi, ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.
Harambee hiyo itazinduliwa na Mwenyekiti wa CCM Taifa, ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambayo inafanyika leo tarehe 12 Agosti, 2025 katika Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news