TCAA yaipongeza TMA kwa huduma bora za hali ya hewa nchini

DODOMA-Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Bw. Salim Ramadhani Msangi ameipongeza, Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kwa kutoa taarifa sahihi na kwa wakati zinazosaidia sekta mbalimbali hususan usafiri wa anga. Ametoa pongezi hizo alipotembelea banda la TMA katika maonesho ya NaneNane kitaifa katika Viwanja vya Nanenane Nzuguni jijini Dodoma.
Bw. Msangi amesema, pamoja na Mamlaka ya Usafiri wa Anga kuwa wadau wakubwa wa huduma za hali ya hewa, huduma hizo ni nguzo muhimu kwa sekta zote kwa vile shughuli nyingi zinaweza kuathiriwa na hali ya hewa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news