Waziri Kombo awasili jijini Yokohama kumwakilisha Rais Dkt.Samia mkutano wa TICAD9

YOKOHAMA-Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb) amewasili jijini Yokohama, Japan kumwakilisha Mheshimiwa Dkt.Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Mkutano wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika (Tokyo International Conference on African Development-TICAD 9) ambao unafanyika kwa ngazi ya Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika na Japan kuanzia tarehe 20-22 Agosti 2025.
Mheshimiwa Waziri Kombo amepokelewa na Mhe. Hideaki Harada, Balozi wa zamani wa Japan nchini Namibia ambaye amekasimiwa jukumu la kumpokea Kiongozi wa Ujumbe wa Tanzania,Balozi wa Tanzania nchini Japan, Mhe. Baraka Luvanda ambaye ameambatana na Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Bi. Felista Rugambwa na Maafisa Wandamizi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Wizara ya Fedha na Ubalozi wa Tanzania nchini Japan.
Mheshimiwa Waziri Kombo pamoja na kushiriki mkutano huo atafanya mazungumzo na Mhe. Takeshi Iwaya, Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan; Bw. Ando Naoki, Makamu wa Rais wa JICA; viongozi mbalimbali wa Serikali na Taasisi wa Japan; Wakuu wa Taasisi na kampuni za uwekezaji wa Japan kwa ajili ya kuhamasisha uwekezaji, biashara na utalii hapa nchini.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news