Waziri Pembe ahimiza amani na usalama kuelekea Uchaguzi Mkuu

ZANZIBAR-Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mheshimiwa Riziki Pembe  Juma amewataka Maafisa, Wakaguzi na Askari wa Jeshi la Polisi kuendelea kuimarisha amani na usalama kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ili uchaguzi huo ufanyike katika hali ya utulivu.
Akizungumza katika hafla ya utoaji wa elimu kwa Mtandao wa Polisi Wanawake pamoja na kuwaaga askari wa kike 27 wanaostaafu kazi kwa mujibu wa sheria, Mheshimiwa Pembe amelipongeza Jeshi la Polisi kwa kuanzisha na kuendeleza mtandao huo na amehimiza ushirikishwaji wa askari wa kike katika kazi mbalimbali za polisi ili kuleta usawa wa kijinsia.
Naye Kamishna wa Polisi Zanzibar, CP Kombo Khamis Kombo amewataka askari wa kike kuendeleza umoja na mshikamano ili kuimarisha Mtandao huo wa Polisi wanawake ambao umekuwa ukileta tija kwa Jeshi Polisi na Jamii.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mtandao wa Polisi wanawake kwa upande wa Zanzibar, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, SSP Pili Fobbe amesema, lengo la kuanzishwa kwa Mtandao wa Polisi wanawake ni kuhamasisha haki na Jinsia ndani ya Jeshi la Polisi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news