Bukombe waonesha mshikamano kuelekea Oktoba 29,2025

BUKOMBE-Wananchi wa Wilaya ya Bukombe mkoani Geita wameonesha mshikamano mkubwa na nia thabiti ya kuendeleza juhudi za maendeleo kwa kutangaza wazi msimamo wao wa kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika uchaguzi ujao wa Oktoba.
Wakiwa wamejipanga kwa kauli mbiu isemayo “Oktoba Tunatiki!”, wananchi hao pia wametangaza kuwa wanamuunga mkono Dkt. Doto Mashaka Biteko, wakimtaja kama chaguo sahihi kwa maendeleo ya Bukombe kutokana na uongozi wake thabiti,wa wazi na wa kisera.

Aidha, wananchi hao wameahidi kuwatiki madiwani wote wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wakieleza kuwa wana imani na ilani ya chama hicho pamoja na utekelezaji wake katika ngazi zote za serikali.

Kauli mbiu kama 
#ChaguaCCM, 
#ChaguaSamia, 
#ChaguaBiteko, 
#OktobaTunatiki, 
#KusemaNaKutenda, 
na 
#KaziNaUtuTunasongaMbele zimeendelea kushika kasi katika majukwaa mbalimbali ya kijamii na mikutano ya hadhara, zikionesha ari ya wananchi kushiriki kikamilifu katika mchakato wa kidemokrasia huku wakitazamia maendeleo endelevu.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news