Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limetoa elimu ya kimazingira na afya kwa vijiji viwili vya Mtonya na Mandela-Likuyu katika Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma kufuatia Mradi wa Uchimbaji wa Madini aina ya 'Uranium' unaotarajiwa kuanza hivi karibuni katika mgodi ulio karibu na vijiji hivyo.
Elimu hiyo imetolewa kwa wananchi kuanzia 8-9 Septemba, 2025 kwa vijiji hivyo huku ikifuatiwa na ukaguzi utakaofanyika katika mgodi huo ikiwa ni hatua ya awali ya kuelimisha jamii na wawekezaji kabla ya Mradi huo kuanza ambapo ni maagizo yaliyotolewa na Serikali ili kuhakikisha jamii inatambua uwepo wa Mradi huo na kuhakikisha jamii haiathiriki na Mradi huo.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo















