Magazeti leo Septemba 16,2025

Zaidi ya watu 5,000 kutoka ndani na nje ya nchi wanatarajiwa kuhudhuria maonesho ya kuku na ndege yanayotarajiwa kufanyika Oktoba 10 hadi 11, 2025 katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.








Akizungumza kuhusu maonesho hayo, Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Uzalishaji Vyakula vya Mifugo Tanzania(TAFMA) na Mjumbe wa Kamati inayoandaa Maonesho ya Kuku na Ndege Wafungwa, Sufian Kyarua amesema maonesho hayo yataambatana na mafunzo kwa wafugaji ili kufanya ufugaji wa kisasa.

“Lengo ni kuhakikisha wafugaji wetu wanaongeza ujuzi na utaalamu ili kuhakikisha wanafunga kwa faida na kuhakikisha mazao yao yanakuwa ni salama kwa walaji.

“Haya ni maonesho ya tisa tulianza 2015 tumekuwa tukipata mafanikio kila mwaka hii inaonesha wafugaji wetu pamoja na walaji wanahamu ya kujua bidhaa tunazozalisha."

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news