Magazeti leo Septemba 18,2025

KIGODA Cha Uprofesa cha Mwalimu J.K. Nyerere katika Taaluma za Umajumui wa Afrika (Chuo Kikuu cha Dar es Salaam) kwa kushirikiana na Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Binafsi (PPP Centre), limeandaa kongamano kubwa la kujadili Uchumi Jumuishi kuelekea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Kongamano hilo litafanyika Septemba 18, 2025 katika Ukumbi wa Nkrumah Lecture Theatre, Chuo Kikuu Mzumbe – Ndaki ya Mbeya, kuanzia saa 5:00 asubuhi, likiwa na lengo la kuwakutanisha wadau mbalimbali kujadili nafasi na fursa za maendeleo ya taifa.

Akizungumza na waandishi wa habari mkoani Mbeya, Mwenyekiti wa Kongamano, Profesa Alexander Makulilo, alisema uhitaji wa kongamano hilo umetokana na kuzinduliwa kwa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Julai 17, 2025 jijini Dodoma.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news