ULIPAJI fidia kwa wananchi waliopisha Mradi wa Gridi Imara umezinduliwa rasmi katika maeneo ya Mkata, Handeni na Kilindi, huku serikali imeahidi kulinda maslahi ya wananchi na kuhakikisha nishati bora inawanufaisha wote.
Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, akizindua zoezi hilo, amesema kiasi cha Sh.Bilioni 1.3 kitatumika kulipa fidia kwa wananchi hao na kueleza kuwa hatua hiyo ni ishara ya kuthamini utu wa mwananchi na uwekezaji alioufanya.
Amesisitiza kuwa jukumu la wananchi sasa ni kulinda miundombinu ya umeme ili manufaa ya mradi huo yaendelee kuwanufaisha vizazi vya sasa na vijavyo.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo














