Magazeti leo Septemba 24,2025

Kampuni ya Kitanzania ya JUSTFIT inayojihusisha na uuzaji na utengenezaji wa vifaa vya michezo kwa kushirikiana na Bodi ya Ligu Kuu Tanzania, imezindua mpira wa kwanza wa Ligi Kuu ambao ni mpira rasmi utakaokuwa ukitumika katika msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Mpira huo ni ubunifu wa Kitanzania ambao umebeba alama ya ubunifu, upekee na ubora wa hali ya juu kwa viwango vya kidunia ambapo uzinduzi wake umehudhuriwa na Salim Salim ambaye ndiye Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya JUSTFIT akiwa na Makamu wa Rais wa TFF, Athuman Nyamlani na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Ligi Kuu,Ibrahim Mwayela.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news