Magazeti leo Septemba 4,2025

Kiongozi wa upinzani nchini Uganda,Kizza Besigye amesusia kikao cha kuanza kwa kesi yake, akisema Jaji ambaye anasikiza kesi hiyo anamwonea na analenga kumhujumu.
Besigye amekuwa kizuizini kwa miezi kadhaa, hali ambayo imezua maswali iwapo Rais Yoweri Museveni kwa kweli anazingatia na kuheshimu haki za kibinadamu.
Museveni anasaka kuchaguliwa tena kwenye uchaguzi wa urais ambao utafanyika mnamo Januari mwaka ujao.

Kesi ya Besigye na msaidizi wake Obed Lutale ilipaswa kuanza Jumatatu baada ya kucheleweshwa kwa miezi kadhaa.

Hata hivyo, wawili hao walisusia vikao vya kesi baada ya shinikizo la kumtaka Jaji Emmanuel Baguma ajiondoe kukosa kuzaa matunda.

Jaji Baguma mwenyewe alikataa kujiondoa katika kesi hiyo kwa mujibu wa wakili wa Besigye Eron Kiiza.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news