Wachezaji wa TAKUKURU Sports Club watakiwa kuendeleza nidhamu na ufanisi SHIMIWI 2025

MWANZA-Katika hatua ya kuwatia moyo, Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mwanza, Bw. Abnery Mganga ametembelea washiriki wa TAKUKURU SPORTS CLUB waliopo katika viwanja vya michezo vya Shule ya Sekondari Bwiro Wavulana, ambako mashindano yanafanyika.
Bw. Mganga amewapongeza kwa hatua nzuri iliyofikiwa, lakini pia aameeleza kuwa, TAKUKURU Mkoa wa Mwanza itaendelea kutoa ushirikiano muda wote kwenye kila jambo ili kuhakikisha timu za TAKUKURU zinafanya vema kwenye SHIMIWI 2025.

Pia,amewataka wachezaji waendelee kujituma na kuendeleza mazoezi ili kuleta ubingwa na kuwa mfano wa kuigwa katika nidhamu ili kujenga taswira chanya ya TAKUKURU

Vilevile, Mkuu huyo wa TAKUKURU Mkoa wa Mwanza amewataka watumishi hao kundeleza mapambano hadi kuchukua ubingwa wa taifa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news