Afisa Msitu wa Suledo wilayani Kiteto hatiani kwa makosa ya rushwa

MANYARA-Mahakama ya Wilaya ya Kiteto mkoani Manyara imemtia hatiani Afisa Msitu wa Suledo wilayani humo,Bw.Siloma Manyindo Mtero kwa makosa ya rushwa.
Taswira ya Msitu wa Suledo wilayani Kiteto. Picha kwa hisani ya Equatorial Initiative.

Hukumu hiyo ya shauri la jinai Na.03/2025 kati ya Jamhuri dhidi ya Afisa huyo imetolewa Oktoba 10,2025 na Hakimu Mkazi,Mheshimiwa Boniface Lihamwike

Katika kesi hiyo, mshtakiwa ametiwa hatiani kwa makosa ya kuomba na kupokea rushwa kinyume na kifungu cha 15 (1) (a) na 15(2) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa sura ya 329 marejeo ya 2023.

Mshtakiwa alitenda makosa hayo kwa kuomba kiasi cha shilingi 600,000 kwa wakulima wa Kata ya Sunya na kuwapa ahadi ya kuwasogezea mipaka ya Msitu wa Suledo.

Lengo ni ili waweze kufanya shughuli za kilimo katika hifadhi hiyo ya msitu, kitendo ambacho ni kinyume na sheria na kanuni za Hifadhi ya Msitu wa Suledo.

Kesi hiyo ilikuwa ikiendeshwa na mwendesha mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU),Bw.Abdulrahim Jamal Mockray.

Mahakama imemtia hatiani na kuamuru kulipia faini ya kiasi cha shilingi 500,000 kwa kila kosa au kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela endapo atashindwa kulipa faini hiyo.Aidha,mtuhumiwa alilipa faini ya shilingi 1,000,000.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news