Magazeti leo Oktoba 12,2025

MKUU wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Kanali Patrick Sawala amemuagiza Mkandarasi M/s Serengeti Limited anayetekeleza mradi wa ujenzi wa Mradi wa Uendelezaji Miji Tanzania (TACTIC) katika Manispaa ya Mtwara Mikindani, kukamilisha kazi hiyo kwa wakati na ubora uliokusudiwa kwa mujibu wa Mkataba ili wananchi waanze kunufaika na miundombinu hiyo inayotekelezwa mkoani humo.
Kanali Sawala ametoa maagizo hayo Oktoba 10, 2025 mara baada ya kushuhudia utiaji saini wa Mradi huo unaohusisha uboreshaji wa miundombinu ya barabara za Chuno na Samia City, mitaro ya kutiririsha maji ya Mvua eneo la Kiyangu, ujenzi wa Kituo kikuu cha mabasi eneo la Chipuputa, Kituo cha wajasiriamali eneo la Skoya pamoja na jengo la usimamizi, mradi utakaogharimu jumla ya shilingi Bilioni 27.49.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news