Magazeti leo Oktoba 19,2025

Polisi katika Kaunti ya Homa Bay wameanzisha uchunguzi kuhusu kisa cha kuteketezwa kwa nyumba ya Mbunge wa Rangwe, Dkt.Lilian Gogo katika Kijiji cha Kotieno usiku wa Ijumaa.
Nyumba hiyo iliteketezwa kwa moto, wakati mbunge huyo akishughulikia mipango ya mazishi ya aliyekuwa Waziri Mkuu, Raila Amolo Odinga,akiwa mwanachama wa Kamati ya Kitaifa ya Mazishi.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Rangwe, Magdaline Chebet, moto huo haukusababishwa na hitilafu ya umeme kwani wakati huo eneo hilo halikuwa na umeme.

“Tumeondoa uwezekano wa hitilafu ya umeme. Moto huu ulisababishwa na mtu aliyeuwasha kwa makusudi,” alisema Kamanda Chebet.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news