Magazeti leo Oktoba 2,2025

Umoja wa Kitaifa wa Asasi za Kiraia wa Shule Salama (NSSC) umetoa rai kwa vyama vya siasa na wagombea nchini kuepuka kuwatumia wanafunzi na watoto katika kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, ukisisitiza kuwa kitendo hicho ni ukiukwaji wa haki za watoto na kinyume cha sheria.
Katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam, wanachama wa umoja huo wamesema kumekuwepo na matukio ya wanafunzi kutolewa darasani kushiriki mikutano ya kampeni, hali ambayo ni hatari kwa usalama, ustawi na haki ya mtoto ya kupata elimu.

Mkuu wa Idara ya Utafiti, Ubunifu na Uchambuzi wa Sera wa HakiElimu, Bw. Makumba Mwemezi, aliyemuwakilisha Mtendaji Mkuu wa taasisi hiyo, amesema ni wajibu wa asasi za kiraia kulinda watoto hususan katika kipindi hiki cha uchaguzi na baada ya uchaguzi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news