Magazeti leo Oktoba 25,2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ametangaza Oktoba 29, 2025 ambayo itakua ni siku ya Uchaguzi Mkuu kuwa ni Siku ya Mapumziko kwa Wananchi wote.
Hayo yamebainishwa kupitia taarifa iliyotolewa Oktoba 24,2025 na Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi Dkt. Moses Kusiluka ambapo ameeleza kuwa, uamuzi huo unalenga kuwapa nafasi Wananchi wote wenye sifa kwenda kupiga Kura ili kutekeleza wajibu wao wa Kidemokrasia.

Dkt.Samia amewasihi wananchi wote kufuata maelekezo na miongozo iliyotolewa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) ili kuhakikisha zoezi la upigaji kura linafanyika kwa amani,utulivu na nidhamu kama ilivyo desturi ya Taifa letu.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news