Temeke waendelea kupiga kura kwa amani na utulivu

DAR-Zoezi la upigaji kura linaendelea kwa amani na utulivu katika Jimbo la Temeke, hususan katika Kata za Vetinari, Tandika, na Makangarawe, ambapo wananchi wamejitokeza kwa wingi kushiriki katika zoezi hilo la kidemokrasia.
Katika Shule ya Msingi Yombo Dovya, wapiga kura wameonekana wakiwa katika foleni wakihakiki majina yao kabla ya kupiga kura, kisha kurejea majumbani mwao kwa utulivu mara baada ya kumaliza mchakato.
Hali kwa ujumla katika vituo hivyo ni shwari, na maandalizi yameonekana kuwa mazuri, huku maafisa wasimamizi wa uchaguzi wakihakikisha kila kituo kinaendesha zoezi kwa ufanisi.
Vikosi vya ulinzi na usalama vimeendelea kuwepo kuhakikisha amani na usalama vinatawala wakati wote wa upigaji kura.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news