TMA yatabiri mvua kubwa mikoa saba

NA DIRAMAKINI

MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya uwepo wa mvua kubwa katika mikoa saba inayotarajiwa kunyesha kuanzia leo.
Mvua hiyo inatarajiwa katika katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani (pamoja na visiwa vya Mafia), Morogoro na Zanzibar.

Kwa mujibu wa taarifa ya TMA, hali kama hiyo pia inatarajiwa kuendelea hadi kesho Jumanne katika mikoa hiyo na kuongezeka hadi maeneo ya Tanga, Kilimanjaro na Arusha.
Aidha,mamlaka imewataka wananchi kuchukua tahadhari na kufuatilia taarifa zitakazotolewa ili kuepuka athari zinazoweza kujitokeza kutokana na mvua hizo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news