Tume yatangaza ratiba ya uchaguzi Jimbo la Fuoni, udiwani Kata ya Chamwino na Mbagala Kuu

DODOMA-Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imetangaza ratiba mpya ya uchaguzi katika maeneo yaliyositishwa kutokana na vifo vya baadhi ya wagombea. Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa leo, kupiga kura katika maeneo husika kutaendeshwa tarehe 30 Desemba,2025.

Uchaguzi huo utahusisha Jimbo la Fuoni, Wilaya ya Magharibi B, Zanzibar, kufuatia kifo cha Kapteni Abbas Ali Mwinyi, aliyekuwa mgombea ubunge kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) kilichotokea Septemba 25, 2025.

Kata ya Chamwino, Jimbo la Morogoro Mjini na Kata ya Mbagala Kuu, Jimbo la Mbagala, ambako pia wagombea wa nafasi ya udiwani walifariki dunia, hivyo kusababisha kuahirishwa kwa uchaguzi katika maeneo hayo.

Tume imesisitiza kuwa uamuzi huu umezingatia masharti ya Kifungu cha 68(1), (3), (4) na 71(2) vya Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya Mwaka 2024.

INEC imewataka wadau wote wa uchaguzi kuzingatia ratiba hiyo mpya na kufuata taratibu za uchaguzi kwa mujibu wa sheria.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news