Comoro yaja kuchota ujuzi Tanzania mapambano dhidi ya rushwa

DAR-Rais wa Taasisi ya Kupambana na Rushwa nchini Comoro (Chambre anti-corruption),Bi Fahamoue Youssouf akiambatana na maafisa wake amewasili Dar es salaam kwa ziara ya kikazi kwa mwaliko wa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU),ndugu Crispin Chalamila.
Ziara hiyo imeratibiwa na Ubalozi wa Tanzania nchini Comoro ambapo Balozi wa Tanzania nchini humo, Mhe. Balozi Saidi Yakubu aliwakaribisha Tanzania na kuwaeleza namna ziara hiyo itakavyokuza ushirikiano katika eneo la utawala bora.
Wakiwa nchini, Bi. Fahamoue Youssouf anatarajiwa kufanya mazungumzo na mwenyeji wake, ndugu Chalamila na kujifunza namna TAKUKURU wanavyofanya kazi na pia kuainisha maeneo ya ushirikiano wa Comoro na Tanzania katika vita dhidi ya rushwa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news