Magazeti leo Novemba 13,2025

SERIKALI imeendelea kuboresha elimu kupitia matumizi ya TEHAMA kwa kuwajengea uwezo walimu wa shule za umma nchini. Kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), hadi kufikia Desemba 2024, walimu 3,798 kutoka shule 1,791 za Serikali za Tanzania Bara na Zanzibar wamepatiwa mafunzo ya TEHAMA.
Mafunzo haya, yanayoratibiwa na Serikali kupitia UCSAF kwa ushirikiano na vyuo vikuu vya UDOM, MUST, na DIT, yamelenga kuwawezesha walimu kutumia teknolojia katika ufundishaji na kutatua changamoto ndogo za vifaa vya TEHAMA vilivyotolewa na Serikali kupitia UCSAF katika shule wanazofundisha.

Hatua hii ni sehemu ya jitihada za Serikali kuhakikisha elimu bora, jumuishi na yenye kuendana na mahitaji ya karne ya kidigitali.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news