Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Camillus Wambura amewataka Watanzania kutokubali kugawanyika kwa sababu yoyote ile, iwe ya kidini, kisiasa au rasilimali na badala yake waendeleze upendo na amani ya taifa.
IGP Wambura aliyasema hayo Novemba 21, 2025 wakati akifunga rasmi Mafunzo ya Awali ya Askari Polisi Kozi Namba 1/2024/2025 katika Shule ya Polisi Tanzania - Moshi, Kilimanjaro.
IGP Wambura amesema amani ya nchi ni jambo la muhimu hivyo kila mmoja anawajibu wa kuendeleza amani na usalama wa nchi ambayo imedumu kwa muda mrefu tangu tumepata uhuru.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo












