Magazeti leo Novemba 26,2025

FAMILIA ya aliyekuwa Waziri Mkuu wa Kenya, hayati Raila Odinga, imeingia tena katika majonzi kufuatia kifo cha mmoja wa wanafamilia wake, Beryl Achieng’ Odinga.
Taarifa za msiba huo zilitolewa Jumanne, Novemba 25, na dada yake marehemu, Ruth Odinga, ambaye alithibitisha kutokea kwa kifo hicho lakini hakutaja chanzo chake.

Ruth alieleza kuwa familia imepokea msiba huo kwa majonzi makubwa, ikisisitiza kuwa wanakubali mapenzi ya Mungu katika kipindi hiki kigumu.
“Ni kwa moyo mzito lakini tukikubali mapenzi ya Mungu, tunatangaza kifo cha ghafla cha Beryl Achieng’ Odinga. Binti wa marehemu Jaramogi Oginga Odinga na Mama Mary Ajuma Oginga. Mama yake Ami Auma, Chizi na Taurus,” alisema Ruth katika taarifa yake.

Beryl Achieng’ Odinga, ambaye anatoka katika ukoo wenye ushawishi mkubwa kisiasa nchini Kenya, amekuwa nguzo muhimu ndani ya familia hiyo, na kifo chake kimetajwa kuwa pigo kubwa kwa wapendwa wake.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news