Matumizi ya vazi la Kanga kuorodheshwa kama urithi wa Utamaduni Usioshikika UNESCO

DAR-Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na wadau imeanza mchakato wa uorodheshaji wa matumizi ya vazi la kanga kwenye orodha ya kitaifa ya urithi wa utamaduni usioshikika, ili kuteuliwa kuingizwa kwenye orodha ya Urithi wa Dunia unaosimamiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).
Mchakato huo umeanza kwa kuratibiwa kwa warsha ya wadau wa utamaduni kutoka Tanzania Bara na Zanzibar iliyofanyika tarehe 11 Novemba, 2025 jijini Dar es Salaam.

Katika warsha hiyo, wadau walipata fursa ya kujadili chimbuko la Kanga na matumizi yake katika miktadha mbalimbali ya kiutamaduni wa Mtanzania na shughuli za kila siku.
Akifungua warsha hiyo, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Maendeleo ya Utamaduni wa Wizara hiyo, Dkt. Julieth Kabyemela amebainisha kuwa, kuorodheshwa kwa vazi la Kanga kama sehemu ya urithi wa utamaduni usioshikika, kutasaidia kuimarisha ushirikiano baina ya Mataifa katika kulinda urithi wa utamaduni usioshikika pamoja na kutangaza utalii wa kiutamaduni kimataifa.
Warsha hiyo imewakutanisha washiriki mbalimbali wakiwamo; wataalamu kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Wizara Ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo-Zanzibar, Ofisi ya UNESCO Dar es Salaam, wahadhiri kutoka vyuo vikuu nchini, asasi za kiraia, sekta binafsi, wawakilishi wa jamii mashirikisho ya kazi za sanaa na Taasisi zilizoko chini ya Wizara.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news