Rais Dkt.Mwinyi kutangaza Baraza la Mawaziri kesho

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, anatarajiwa kutangaza rasmi Baraza Jipya la Mawaziri katika hafla fupi itakayofanyika Ikulu Zanzibar, kuanzia saa 4:00 asubuhi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Mheshimiwa Dkt.Hussein Ali Mwinyi.

Hafla hiyo itahudhuriwa na wahariri pamoja na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali, ambapo Rais Dkt. Mwinyi atalitambulisha Baraza hilo pamoja na wizara zake. Tukio hilo pia litangazwa moja kwa moja kupitia vyombo vya habari nchini.

Aidha, Rais Dkt. Mwinyi atazungumzia mwelekeo wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kutekeleza vipaumbele vyake, vikiwemo Uchumi wa Buluu, Uwekezaji, Huduma za Jamii, Miundombinu, na Maendeleo Jumuishi kwa Wananchi.

Mawaziri watakaoteuliwa wataapishwa siku ya Jumamosi ya Novemba 15, 2025 saa 8:00 mchana, katika viwanja vya Ikulu Zanzibar ikiwa ni hatua muhimu inayoashiria mwanzo wa safari ya Kipindi cha Pili cha Serikali ya Awamu ya Nane.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news