Chuo cha Ustawi wa Jamii chatwaa tuzo ya Uandaaji wa Hesabu kwa Viwango vya Kimataifa vya Uhasibu wa Sekta ya Umma kwa mara ya nane

DAR-Naibu Mkuu wa Taasisi Mipango, Fedha na Utawala, Dkt. Zena Mnasi Mabeyo akipokea tuzo ya Uandaaji wa Hesabu kwa Viwango vya Kimataifa vya Uhasibu wa Sekta ya Umma (International Public Sector Accounting Standards (IPSAS), kundi la Vyuo vya Elimu ya Juu Tanzania.
Katika tuzo hizo Chuo cha Ustawi wa Jamii kimeibuka mshindi wa tatu,ikiwa ni mara ya nane mfululizo toka mwaka 2017 ambapo ISW inashika nafasi za juu kwenye mashindano hayo.
Naibu Mkuu wa Taasisi aliambatana na Mhasibu Mkuu, Aisha Kapande Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu za Ndani kutoka Chuo cha Ustawi wa Jamii.
Tuzo hizo zimetolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) usiku wa tarehe 04/12/2025 katika ukumbi wa APC Bunju, jijini Dar es Salaam.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news