Magazeti leo Desemba 20,2025

Tume Huru ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, mwaka huu, imekutana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila na kujadili mambo mbalimbali yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi huo.
Kikao hicho kilifanyika Desemba 18, 2025 kwenye ofisi za muda za tume hiyo jijini Dar es Salaam, ambapo Chalamila aliambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Tume hiyo chini ya uenyekiti wa Jaji Mkuu mstaafu Mohamed Chande Othman, imeundwa na Rais Samia Suluhu Hassan, ikiwa na wajumbe wengine saba ambao ni Watanzania wabobezi katika masuala mbalimbali.

Majukumu ya tume hiyo ni pamoja na kuchunguza chanzo cha matukio ya Oktoba 29, mwaka huu, kubaini waliohusika, kutathmini madhara yaliyojitokeza na kupendekeza hatua za kuimarisha amani, usalama na umoja wa kitaifa.

Tume imewaita wananchi watoe taarifa, ushahidi, maoni na mapendekezo yatakayosaidia katika uchunguzi wake.

Kwa mujibu wa Jaji Mkuu mstaafu Chande, mafanikio ya kazi hiyo yatategemea ushirikiano wa wananchi wenye taarifa zinazoweza kusaidia kubainisha ukweli.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here