Magazeti leo Desemba 27,2025

MBUNGE wa Jimbo la Mtumba na Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, amemkabidhi nyumba iliyofanyiwa ukarabati Bi. Verian Mlewa mwenye umri wa miaka 75, mkazi wa Kata ya Mtumba jijini Dodoma, ambaye alikuwa katika hatua ya kuiuza nyumba yake kwa Shilingi 500,000 ili kupata fedha za matibabu baada ya kuugua uvimbe katika ubavu.
Hatua hiyo imefuatia taarifa za hali ya bibi huyo kuripotiwa kwenye vyombo vya habari, ambapo kwa kushirikiana na Kitengo cha Ustawi wa Jamii, Bi. Verian alipelekwa Hospitali ya Rufaa ya Dodoma na kufanyiwa upasuaji uliomwezesha kurejea katika hali nzuri ya afya.

‎Akizungumza na wananchi wa Mtaa wa Vikonje B, Kata ya Mtumba, wakati wa kukabidhi nyumba hiyo Desemba 26, 2025, Mhe. Mavunde amesema kuwa aliguswa na simulizi ya maisha ya bibi huyo baada ya kuona taarifa zake kwenye vyombo vya habari.

‎“Nimeona nitumie fursa hii kuikabidhi nyumba iliyofanyiwa ukarabati. Nyumba hii ni ya Bi. Verian aliyeijenga mwenyewe. Baada ya kuona taarifa kuwa anaumwa na kukosa fedha za matibabu hadi kufikia hatua ya kutaka kuuza nyumba yake, tulishirikiana na ofisi ya ustawi wa jamii kumpeleka hospitalini, akafanyiwa upasuaji na kupona,” amesema Mhe.Mavunde.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news