Polisi Utalii na Diplomasia,Idara ya Uhamiaji mbioni kuanzisha Kituo cha Pamoja

ARUSHA-Mkuu wa Kituo cha Polisi Utalii na Diplomasia Mkoa wa Arusha, Mrakibu wa Polisi SP Waziri Tenga amesema Kituo hicho kwa kushirikiana na Idara ya Uhamiaji wamepanga kuanzisha kituo cha huduma kwa saa 24 chenye lengo la kuboresha na kuharakisha huduma kwa watalii na wageni.
SP Tenga ameyasema hayo leo Disemba 21, 2025 wakati alipokua anazungumza na waandishi wa habari ambapo amebainisha kuwa kituo kilichopendekezwa kitawawezesha watalii kupata huduma muhimu ikiwa ni pamoja na usaidizi kwa wale wanaopoteza hati za kusafiri kwa haraka.

Mkuu huyo wa Kituo aliendelea kufafanua kuwa kwa sababu watalii wanaingia na kutoka nchini kila wakati, kituo hicho kitakuwa kinatoa huduma kwa saa 24 kila siku bila kujali siku za sikukuu.

Katika hatua nyingine alibainisha kuwa Jeshi la Polisi mkoani humo limeimarisha usalama hususani kwa watalii na wageni wanaofika mkoani humo kupitia doria mbalimbali ikiwemo za mitandaoni na maeneo wanakofikia watalii.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news