Taarifa muhimu kutoka Jeshi la Polisi Tanzania

TAARIFA KWA UMMA

Kuna hii taarifa upande wa kushoto iliyotengenezwa kwenye mfumo wa sauti na mwanamke na inasambazwa kwenye mitandao ya kijamii.
Jeshi la Polisi linaendelea kueleza katazo la kutokufanyika kwa kinachoitwa maandamano ya amani lililo tolewa jana Disemba 5,2025 lipo pale pale kwa sababu za kisheria ambazo hazijafuatwa na mbinu za kihalifu zinazopangwa sambasamba na maandamano hayo.

Jeshi la Polisi linaendelea kutoa wito kwa wananchi wakatae uhamasishaji, uzushi na uchonganishi wa aina hii na mwingine ambao lengo lake ni kuleta vurugu itakayo vuruga amani na usalama wa taifa letu.

Aidha, Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama vinaendelea kuwahakikishia wananchi wote wafuata sheria, wapenda amani, usalama wa taifa letu na wasiopenda kuchonganishwa na wanaopenda kutatua changamoto kwa busara, mazungumzo, maridhiano, maelewano na mshikamano wa kitaifa kuwa vipo tayari wakati wote kuwalinda siku zote.

Imetolewa na;
Msemaji wa Jeshi la Polisi
Makao Makuu ya Polisi
Dodoma,Tanzania

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news