Tuwafichue wahalifu waliopo katika maeneo yetu

KATAVI-Wananchi wa Kata ya Mwamkulu Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi, wametakiwa kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kuwafichua wahalifu waliopo katika maeneo yao ili kuimarisha usalama na kudumisha amani katika jamii.
Wito huo umetolewa leo Disemba 12, 2025 na Mkuu wa Polisi Jamii Mkoa wa Katavi, Mrakibu wa Polisi John Mwaipungu wakati akitoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kushiriki kikamilifu katika mapambano dhidi ya uhalifu, ikiwemo kutoa taarifa mapema wanapobaini viashiria vinavyoweza kuhatarisha usalama katika maeneo yao.
SP. Mwaipungu amesisitiza kuwa ushirikiano baina ya wananchi na Jeshi la Polisi ni msingi muhumu wa kuimarisha ulinzi shirikishi akiwataka wananchi kuendelea kuwa walinzi wa kwanza wa maeneo yao na kutofumbia macho vitendo vya kihalifu vinavyojitokeza.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news