Wahimizwa kuendelea kudumisha amani na usalama

TANGA-Wananchi wa Kijiji cha Kitivo, Kata ya Lushoto, Wilaya ya Lushoto Mkoa wa Tanga wamehimizwa kushiriki kikamilifu katika kudumisha amani na usalama katika maeneo yao.
Wito huo umetolewa Desemba 25,2025 na Inspekta Karim Bruno, wakati wa zoezi la ushirikishaji jamii lililofanyika katika Kitongoji cha Kitivo, Kata ya Lushoto, Wilaya ya Lushoto.
Katika utoaji wa elimu hiyo, wananchi wameaswa kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu mara moja pindi viashiria vinapojitokeza, kupinga vikali ukatili na unyanyasaji wa kijinsia na watoto, pamoja na kuacha kujihusisha na biashara haramu za pombe aina ya moshi na dawa za kulevya ikiwemo bangi.
Wananchi wa Kijiji cha Kitivo wameishukuru Jeshi la Polisi kwa elimu waliyopewa na kuahidi kuendelea kushirikiana na Polisi katika kulinda amani na usalama wa maeneo yao.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news