Askofu Prosper Lyimo ateuliwa kuwa Askofu wa jimbo jipya la Bariadi

ROME-Januari 8,2026 Mkuu wa Kanisa Katoliki Duniani,Baba Mtakatifu Leo XIV amemteua aliyekuwa Askofu msaidizi wa Jimbo Kuu Arusha, Mhashamu Prosper Baltazar Lyimo kuwa Askofu wa kwanza wa Jimbo jipya la Bariadi.
Askofu Lyimo alizaliwa Agosti 20, mwaka 1964 ambapo baada ya masomo ya kipadri alipewa Daraja Takatifu la Upadre mnamo Julai 04 mwaka 1997 jimboni Arusha.

Askofu Lyimo ambaye ana shahada ya uzamivu (PhD) katika sheria za Kanisa, alikuwa Askofu msaidizi wa Jimbo Kuu la Arusha tangu mwaka 2015.

Tarehe ya kusimikwa rasmi kwa Askofu Lyimo kuwa Askofu wa kwanza na mwanzilishi wa Jimbo jipya la Bariadi, itatangazwa hapo baadaye.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here