Magazeti leo Februari 27,2026

Serikali imeanza rasmi utekelezaji wa mpango wa ufadhili wa Shahada ya Uzamili katika Sayansi ya Takwimu, Akili Unde (AI) na Sayansi Shirikishi chini ya Samia Scholarship Extended (SSE DS/AI+), hatua inayolenga kuimarisha rasilimali watu katika sekta ya sayansi na teknolojia nchini.
Katika awamu ya kwanza, wanafunzi 10 wamepatiwa ufadhili huo na watajiunga na masomo katika Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, huku wengine 10 wakitarajiwa kuanza masomo yao katika Indian Institute of Technology Madras Zanzibar Campus.

Akizungumza na waandishi wa habari Februari 25, 2026 jijini Dodoma, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, amesema uwekezaji huo ni mkakati wa Serikali kukidhi ongezeko la mahitaji ya wataalamu wa takwimu, akili unde na teknolojia bunifu.

Amebainisha kuwa jumla ya Sh bilioni 5 zimetengwa kugharamia mpango huo, akisisitiza kuwa ni sehemu ya dhamira ya Serikali ya kujenga uchumi wa maarifa unaotegemea sayansi na ubunifu.

Prof. Mkenda ametoa wito kwa wadau kushirikiana na Serikali kwa kuchangia mfuko wa Samia Scholarship, huku akiwataka wanafunzi waliopata ufadhili wa Shahada ya Kwanza kupitia mpango huo kuangalia majina yao kwenye tovuti za Wizara, Tume ya Sayansi na Teknolojia Tanzania pamoja na Taasisi ya Nelson Mandela.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here