BoT yasaini hati za makubaliano ya kimkakati kuhusu Akili Unde na Ubunifu wa Data

Makubaliano haya yanalenga kukuza matumizi ya akili unde, ubunifu katika matumizi ya data, na tafiti katika kuongeza tija kwenye uundaji wa sera na usimamizi wa sekta ya fedha.
Aidha, makubaliano hayo yana viambatisho vinavyohusisha Itifaki ya Ushirikishwaji wa Data, ambapo BoT itatoa data zilizozingatia Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, ili kuwawezesha watafiti vyuoni kupata uzoefu wa kutatua changamoto halisi, kupunguza muda wa utafiti unaosababishwa na ukosefu wa data, na kukuza ubunifu katika akili unde na matumizi ya teknolojia za kisasa za data.
Gavana wa Benki Kuu amesema tukio hili ni hatua ya kimkakati katika kuimarisha ubunifu unaozingatia maadili, usalama na maslahi ya umma.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here