Magazeti leo Januari 4,2026

Familia ya Juma Maganga imemshukuru Waziri wa Madini na Mbunge wa Jimbo la Mtumba, Mhe. Anthony Mavunde kwa kumsaidia mtoto wao kuachiwa huru kufuatia tukio lililotokana na ajali ya barabarani.
Ajali hiyo ilitokea Februari 14,2025 nchini Sudan Kusini, ambapo Juma Maganga, aliyekuwa dereva wa gari kubwa, alimgonga mwanajeshi mmoja aliyepoteza maisha. Tukio hilo lilisababisha Juma kushikiliwa na vyombo vya sheria vya nchi hiyo.

‎Juma Maganga alitakiwa kufanya malipo ya dola za Kimarekani 1,500 katika Mahakama ya Juba, Sudan Kusini. Desemba 29,2025, Mhe. Anthony Mavunde alifanikisha hatua hiyo ya malipo, hatua iliyofungua njia ya kuachiwa kwa Juma Maganga.

‎Aidha,Desemba 31,2025, Juma Maganga aliachiliwa huru na kuanza safari ya kurejea nyumbani Dodoma, Tanzania ambapo aliwasili Januari 3,2026 na kupokelewa nyumbani.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here