Polisi waanza uchunguzi kipigo kwa watu wawili

NA DIRAMAKINI

JESHI la Polisi limesema limeanza kuchunguza wa kina picha mjongeo ambayo inaonesha watu wawili wakipigwa kitendo ambacho ni kinyume cha sheria na haki za binadamu.
Jeshi hilo limesema uchunguzi huo umeanza ili kubaini anayefanya kitendo hicho ni nani, wanaofanyiwa ukatili huo ni akina nani, ulifanyikia wapi na lini ili hatua stahiki na za haraka za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi ya mhusika.

Aidha, Jeshi la Polisi linatoa wito kwa yeyote mwenye taarifa za kuweza kusaidia kumbaini aliyekuwa anafanya ukatili huo, atoe ushirikiano.

Pia, waliokuwa wanafanyiwa ukatili huo nao wajitokeze kwa kiongozi yeyote wa Polisi au kwa watakayemwona ni rahisi kwao ili kufanikisha kukamatwa kwa aliyekuwa anawafanyia kitendo hicho kilicho kinyume na sheria.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here