Utabiri tata wa mwisho wa Dunia wazua taharuki,Nabii akamatwa

ACCRA-Jeshi la Polisi nchini Ghana limemkamata Nabii Evans Eshun maarufu kama Ebo Noah, baada ya utabiri wake wa kudai kuja kwa mwisho wa dunia kusababisha hofu kubwa miongoni mwa wananchi.
Nabii Eshun alidai kuwa, dunia ingeangamia siku ya Krismasi mwaka 2025 kupitia mafuriko makubwa, akieleza kuwa ni wale pekee watakaokuwa ndani ya majengo aliyoyaita “safina nane” ndio wangepona. Kauli hiyo ilizua taharuki na mjadala mpana ndani na nje ya nchi.

Kwa mujibu wa polisi, Eshun alikamatwa na Kikosi Maalumu cha Ukaguzi wa Mtandaoni chini ya Ofisi ya Inspekta Jenerali wa Polisi, kama sehemu ya juhudi za kudhibiti matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii na shughuli za mtandaoni, hususan kuelekea ibada za kidini za mkesha wa Mwaka Mpya.

Utabiri huo ulisambaa kwa kasi nchini humo kupitia mitandao ya kijamii, na kuchochea hofu, maswali na hisia kali kutoka kwa wananchi na watumiaji wa mitandao mbalimbali.

Polisi wamesisitiza kuwa,hatua zilizochukuliwa zinalenga kulinda usalama wa umma na kuzuia taarifa potofu zinazoweza kuhatarisha utulivu wa jamii. (NA)

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here