DAR-Kamati ya Kitaifa ya Usalama wa Usafiri wa Anga (NCASC) imefanya kikao chake cha 64 jijini Dar es Salaam, Februari 3, 2026 katika Makao Makuu ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), kwa lengo la kujadili masuala muhimu yanayohusiana na usalama wa usafiri wa anga nchini.
Kikao hicho cha siku moja kimeongozwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Bw. Salim Msangi na kimehudhuriwa na wajumbe wa Kamati hiyo kutoka sekta mbalimbali zinazohusiana na Usalama wa Usafiri wa anga nchini.Kamati hiyo ya Kitaifa ina jukumu jukumu la kuishauri Serikali katika masuala ya kiufundi, sera na hatua za kuboresha usalama wa usafiri wa anga nchini, pamoja na kuhakikisha kuwa shughuli zote za usafiri wa anga zinazingatia viwango vya kitaifa na kimataifa vya usalama.


